Jump to content


MTU WA KWELI


13 replies to this topic

#1 quertzal

    Advanced Member

  • Members
  • PipPipPip
  • 49 posts
  • Locationkimara maskani

Posted 15 April 2005 - 09:54 AM

Sikai meza moja na wanafiki/wanakenua meno ujue marafiki/dhiki zimewajaa nyoyo zimesheheni chuki/wanaoneaka smart kumbe nyuma wameficha bunduki/mc sasa ngangari mwanzo mpaka mwisho wa week/nimekuwa mtu wa kweli/yaani natumia akili maarifa yakizidi mwili/ nabadilisha nyendo bila kupoteza asili/ ujuzi na mbinu zangu zanifanya jasiri/kama unata battle tukutane wawili na siku tam ni jumapili/ hapa nipo kwa wito na si kufuata ujiko/nang'arisha popote mlipo baharini mito mpaka vijito/rhymez zina mvuto usafiri wangu bito kamwe si vunji miiko na mziki wangu mzito/ sipendi propaganda enyi nyote nawasabai/ sitaki makuu napanda Punda ili wa chini niwape hi/ nakata ngebe kimtindo midoshoo nawapa dry//siitaji nguvu ya kilevi/ ili kwenye stage nionekane heavy/si chagui sibagui nitawarusha wenye jealous na envy/mc nang'ara mashariki ya mbali mpaka kimara/ si chagui biashara/ sitaki ujiko kwenye radio uchwara/Big up knifebutcher waelimishe uku ukiwarusha/salaam Alcapaino battle zako hazina mfanooo


Lyrica Blower!

Quertzal
"Guys don pretend keep it real so dat kids can learn n grow from us"

Quertzal a.k.a lyrical blower

#2 skywalker

    Advanced Member

  • Members
  • PipPipPip
  • 35 posts
  • LocationFrom the hood

Posted 17 April 2005 - 10:23 AM

Amani tena hakuna mbabe anapovuma/
MC mwenye nguvu usoni kavaa chuma/
Kwa mtindo braza utazidi kubaki nyuma/
Kupisha ndo utapisha simba akiunguruma/
Rhymes zako kinda,kama mtoto we kitinda mimba/
Usisite kuniamkia ukipenda niite mjomba/
Ukitaka we nifuate bure kurap ujifunze/
Kama hunijui mi ndo sky,mc natamba hewani/
Karibu kwenye mkondo najongea nishike chati::::::

#3 quertzal

    Advanced Member

  • Members
  • PipPipPip
  • 49 posts
  • Locationkimara maskani

Posted 20 April 2005 - 01:24 PM

Watu wa mjini ndio wa kwanza kuliona jua//
nafikiri hili wewe bwana mdogo wa bush bado tambua//
na ni sisi tunawakilisha na kufanya nyinyi ki-mc mpate kukua//
sasa unatukana wakunga je hiyo mimba utajifungua??//
hichi kichwa kimejaa thawabu na hekima za ki-mababu//
uki-battle babu hapa aibuuu na maisha yako ki-mc yatakuwa ya taaaabu//
naona unajaribu traatiibu kukwea merikebu iliyojaa waarabu//
mikono yako laini utaishia chezea tuu zangu sharubu//nitakupa hifadhi na moja ya vazi lako binti skywalker itakuwa ijabu//
natumia nguzo na itikadi zenye misimamo//si fanyi tuu vijimambo watu kama nyinyi mpate msemo//natoa ujuzi ikibidi niletee demo//
nabadilika kutokana na mingi yangu ya maisha mifumo//najua huwezi kujifunza bila kuchafuka njoo hapa nitakuogesha kwa omo//mimi ni sebby a.ka. quertzal mind blower//mbona huna hema si ulikuja moto hapa umepoaa//nimekata yako kauli nimekuacha unakoa//
quertzal n knifebutcher ndio wazee saluti mpaka kwa machangu doa//

kama kawa//
Mind blower//
Quertzal//
"Guys don pretend keep it real so dat kids can learn n grow from us"

Quertzal a.k.a lyrical blower

#4 skywalker

    Advanced Member

  • Members
  • PipPipPip
  • 35 posts
  • LocationFrom the hood

Posted 21 April 2005 - 03:43 AM

Bila shaka bwan'mdogo unaiamini methali hii ya chini/
Kwamba jogoo la shamba haliwiki mjini/
Nataka nioneshe mapinduzi makali kiasi usiamini/
Umemchokoza mbogo lindoni,Ingekuwa vema ukakaa kibindoni/
Kamwe sitapata huruma kukufukia shimoni/
Umeyavulia mweyewe maji sharti uyaoge bafuni/
Mi ndo sky kama msunni naingia vitani/
Ninapochokozwa kamwe dunia haina amani/
Eti sebby wa kimara unataka yangu nishani/
Au nikupe box ya mdomo utokee dirishani/
Pengine nitoe mahari nikuokoe maishani/
Wapendeza binti kijana eti we kabila gani/
Mi kwetu kukatana mapanga si jambo geni asilani/
Nashangaa mtoto wa mama unanilazimisha niingie hasirani/
Ni bora mwenzio knife bucha ukweli ameubaini/
Kafyata mkia, na heshima utadhani kawekewa plasta mdomoni/
We ndo bado naandaa dawa yako jikoni/
rhymes ndo silaha harafu ndo hivyo ziko pomoni/
Angalia kwenye battle za lugha ya kimombo/
Uone jinsi sky nilivyoinyanyua Bongo/
Nimekomaa na machizi wa huko ng'ambo/
Na sasa P kubwa, wamegundua kuwa mi ndo mtambo/
Kwanini hunipi heshima mimi kaka yako/
Nikufundishe kuimba rap uwashinde adui zako/

Any mshikaji waingereza husema:OPPORTUNITY COMES ONCE IN LIFE TIMES,mimi nishazeeka mdogo wangu, tumia muda huu nikurithishe mikoba ya sanaa utoke mpaka lini utaka unakomaaa,Aiseee unachekesha.teeeeeh..teeeeeeeeeeeeeeh.

#5 quertzal

    Advanced Member

  • Members
  • PipPipPip
  • 49 posts
  • Locationkimara maskani

Posted 21 April 2005 - 10:05 AM

Bwana mdogo hii tsunami//unataka kuburuzwa chogo hii kambi ya army//
naona unatema fyongo huyu ni quertzal 120 hata kona za mto wami//
rudisha kikosi nyuma pindi pale upepo wangu unapo vuma//
huwa sina huruma/nachakaza kizazi chenu maendeleo narudisha nyuma//
unacheza na nyati wakati hauna shati//ni sawa kupiga kelele jukwani bila kipaza sauti//ukija mjini njoo smart lakini husi chomekee suti//jipulizie perfum husije unanuka hudi//umepita mtaa wa magaidi/utachokozwa ikibidi hata kwa maksudi//wewe ni kinyama cha mwitu halali ya mafisadi/
kama unapenda beef qurtzal hapa sheriff//kama unataka utiifu hiki kichwa cha chief//si pendi vita na wenye game dhaifu//uwa nazoa point bila kufika uwanja wa beef// nina jeshi zaidi ya siafu sijali wewe ni mwana ccm au cuf//inavutia mc wa musoma mtandao unapokuunganisha na sisi watu wa dunia//bado kitu kimoja rhymes zako hazija simama hilo staacha kukuambia//anyway keep hooked na mazoezi mengi yatakuinua//hii ndioo dunia quertzal 4life AMINIAAAAAAAAA!!!!!

Mind blower!!
Quertzal!!

Knifebutcher yupo kiwanja mara moja hata kwenye ndoto atakuzukia don worry keep cloz to ur short.
"Guys don pretend keep it real so dat kids can learn n grow from us"

Quertzal a.k.a lyrical blower

#6 skywalker

    Advanced Member

  • Members
  • PipPipPip
  • 35 posts
  • LocationFrom the hood

Posted 22 April 2005 - 03:35 AM

Qurtazal mdogo wangu hivi huogopi moto wa gesi/
Au tu unamind kaka yako nishikiliwe kwa kesi/
Ungekuwa unajua ungeufunika mdomo wako upesi/
Mi ndo stone cold nashangaa unaleta kibesi/
Kama game ni hospitali mi ni Dokta we ni nesi/
Mbona hunyamazi wakati unajua i'm expected no mercy/
Umesema umekodi jeshi harafu unamleta huyo kibonde/
Usikonde,mtu single kama tangawizi mi niwaponde/
Nakushangaa sana mdogo sebby,umekodi mwimbaji au mchemkaji/
Juzi katoka nursery ati naye a-battle na mf***ji/
Hapa no stop,mashambulizi mpaka uzeeni/
Na rise to the stop,wachovu wachovu njia iachieni/
Navaa nguo za cop,watuhumiwa nyie sambaeni/
Si bongo flava ni kwa rap,najaa ulingoni/
Na hizi rhymes na zidrop,mpaka masikioni/
Eyo eyo navyo blaze,wachovu hatiani/
Sifanyi mchezo na wash**zi,wasio makini/
Hebu kamata kisha nata na mkia fyata/
Sifanyi battle na msanii anaeng'ata/
Wenye akili wamejitoa na hili sakata/
Wameshahisi moto mkali ujinga wameachaaaa..

Hey little boy, u better warn dat Bitch,before I break his mouth,Im not as simple as he thinks I might be,tell him fu** off.

#7 Mchapakazi

    African Hip Hop Regular

  • Members
  • 213 posts
  • LocationDeventer, Holland

Posted 25 April 2005 - 06:49 AM

Hakuna kitu kamwe uwezi kuwa emcee wa kudumu/
mchovu kimashairi kama mgonjwa wa pumu/
I treat ya like mchumba nunu/
nakupa kichapo alafu kama Ali Chemical nakumwagia silaha za sumu/*
ati ng'ambo ass whole unakaa Tarime au Mugumu?/
alafu unaingia ovyo anga za wagumu/
nitakujaza mashairi waungwana wakuhukumu/*
Kwenye L waweka R na R waweka L lini kiswahili kimekua lugha ngumu?/
ushamba umekuganda brother tena wa kudumu/
lete bia mbili ushakuwa kama simba wa bar muhudumu/
tunapoteza wajinga kama nyie ili hip hop idumu/*
nasikia huko gongo kwa vidumu/ hali ya maisha ngumu/
utaweza wapi kusplit wakati daily wanywa chi/kimpumu/*
heri ndumu/
so Son watch ya steps this is more official punk....../*
Bitches are like tornadoes scream when they come,and take everything when they leave

#8 skywalker

    Advanced Member

  • Members
  • PipPipPip
  • 35 posts
  • LocationFrom the hood

Posted 26 April 2005 - 08:35 AM

84 ndo umezaliwa wakati sky std seven ndo nahitimu/
Huoni tofauti kubwa kati ya chungwa na ndimu/
Tanzania watoka sehemu gani Muleba ama kamachumu/
Mbona adabu huna unaropoka kama binti fulani aitwa kuruthumu/
Pengine tukupe sketi ubadili jina uitwe mwatumu/
Toka ujue kuvaa chachacha kaunda suti na njumu/
Hutaki kabisaa kuambiwa mitkasi fulani ya muhimu/
YAH ni kweli life la huku mjomba watoto walegevu haliwafai/
Wewe na mabishoo wenzako mlozea asubuhi tu chai/
Nivigumu kustahimili labda mahardcore akina Sky/
Watu wa huku wamepinda hawafagilii kabisa maspy/

Whatch out kid.......

#9 Mchapakazi

    African Hip Hop Regular

  • Members
  • 213 posts
  • LocationDeventer, Holland

Posted 27 April 2005 - 05:17 AM

Yoh Yoh one two three to da four/
asubuhi ya J4/ nashusha free flow/
najua uwezi maana we bishoo/
we I do ma show/ for u is big blow/
niko makini kama GURU au Curtis blow/
vina bora vitavyokuamisha ulipo kuja kariakoo/
mjomba hapa ni so/
najua nimekukaba koo/
na sasa naona unasound down low/
hamia kidali poa/ hama promo za ukimwi na wala usione soo/
nilikuwa Compton na NWA the yr ya mention, yeah it was eighty four/
hivyo hapa sky punguza mapepe na uje slow/
maana kama life tough hivyo, that means u don't have dough/
jitaidi kuuwa soo/ bongo yako hiyo, usije osha choo/
kaza kaza basi hata kwa siku online mara moja njoo/
Reply unipe hamasa/ kaka
nikupe mashairi ya kutakata/
yakuoshe kuliko sadaka/
maana robo tatu unaflow taka/
that's tru kaka/ usije sema napaka/
kama umenunu sema nyau kama paka



IMAO
Bitches are like tornadoes scream when they come,and take everything when they leave

#10 quertzal

    Advanced Member

  • Members
  • PipPipPip
  • 49 posts
  • Locationkimara maskani

Posted 28 April 2005 - 11:53 AM

Nimeshakuteka bwana mdogo kama ibilisi//
akili, fikra,mawazo yako quertzal amefilisi//
haufai kuguswa umesheheni nuksi// hichi kichwa kiite quertzal a.k.a kamusi//
huna ladha,thamani,damu ilishanyonywa na quertzal chunusi//
mjane skywalker umebaki msusi//
umiza kichwa,natuliza akili kama unacheza chess//
kidaraja niite askofu wewe bado shemasi//
huna pa kujibanza ki-mistari sebby nasaza//
ki -hiphop ushachakazwa quertzal kote nameza//
huna nafasi mjomba iliyobaki ya mke wenza//
ushazoea kuoga porini wapi utaweza jaquuz??//
hili jiji kila cku lakupa njozi tak care utapata uchizi//
haya nayaweka wazi kijakazi husipate simanzi//
dawa si fumanizi wala irizi ujibu quiz//
unacheza na wachapakazi/ kwa chai ya rangi na moja andazi??//
hizi style kamakazi zakupa njoozi//
zikikutafuna ki-mapozi na zikikuchapakazi//

Mind Blower!
Quertzal.
"Guys don pretend keep it real so dat kids can learn n grow from us"

Quertzal a.k.a lyrical blower

#11 Mchapakazi

    African Hip Hop Regular

  • Members
  • 213 posts
  • LocationDeventer, Holland

Posted 28 April 2005 - 01:00 PM

mueleze atambue kwamba hip hop kazi/
ajitaidi kupanda ngazi kwa ngazi/
sio kurukia tu asije pata razi/
na misingi ni vina, mashairi pamoja na mavazi/*
usije kujaza shazi/ na kushusha hadhi/
hii forum na ya wanahip hop sio mabazazi/
angalia Sky kuna tofauti kati ya dafu na nazi/*
we si msanii ni paparazi/
hata kwenye lines tunaweza kubig up kwa new Papa Ratz/
kughani kwangu time yoyote hiyo iko wazi/
popote naongoza jahazi toka north mpaka Sauzi/*
Ona sasa umekimbia/ nasikia unalia/
kisa wamekuanzishia gwarida la kushoto kulia/
hii ngome utaadithia/ pia/*
maana fake MC's ndipo walipofia/
kama kiwanja mimi Amsterdam Schipol, wewe Kia/
nakuona unavyoofia/ na ndio maana kila siku unashika mkia/*


Watch ya out Son, I can give lil tip in writing skills, holla....
Bitches are like tornadoes scream when they come,and take everything when they leave

#12 skywalker

    Advanced Member

  • Members
  • PipPipPip
  • 35 posts
  • LocationFrom the hood

Posted 30 April 2005 - 04:53 PM

Ilikuwa ni likizo tyme nikila happy na shemeji yenu/
so im back turhyme tugongenishe zangu na zenu/
4 REAL nawakilisha hippop tofauti na yenu mayenu/
AU muziki fulani wa huko kwa kina iwe mbwenu/
sijakimbia niko stead kama Al-zarkawi/
mi ndo mti bwana washamba bakieni matawi/
rap si tunguri madogo siamini uchawi/
Is all about talent iwe bongo hata malawi/
nafunika kwa fujo najua mlidhani hayawi/
Nicheki niko tîght mazeee ebana eeeee/
narule kwa stye aisee ova kamikazeee/
starling kwenye movie,nafight mtoke ushuzi/
pruuu :lol: kama kazi roba za mbao ustaadh.........

im still blazing...........an welcomin you kids

#13 Knifebutcher

    African Hip Hop Regular

  • Members
  • 112 posts
  • LocationSouth Africa

Posted 01 May 2005 - 10:27 AM

nacross kama kete lazima unicrown ukingi
kama rymes ni shule we bado uko msingi
kama ni umri basi we unatambaa na mimi ni dingi
kivipi unajaribu kupambana na vigingi
kigezo cha uemcii sio kuwa na miverse mingi
lakini we poyoyo mpaka mida hii hujanielewa
ngoja nianzee kukuburuza kama behewa
nitakuacha ussafocate kwa kukosa hewa
hapa ni mchaka mchaka tuu yaani kindewa ndewa

oya we dogo wa musoma huchikii wewe :evil: :evil:

#14 quertzal

    Advanced Member

  • Members
  • PipPipPip
  • 49 posts
  • Locationkimara maskani

Posted 10 May 2005 - 01:08 PM

Vipi kijana sky mbona sana midomo unachonga//
huna mpya naona kwa wanaume sasa wajigonga//
ni quertzal kidume wewe hapa ni shoga//
husije kwa woga na meno kuchonga hapa utafanywa boga//
hivi ni wewe kijiba fyuzi mtoto wa juzi juzi//
uliyepata tuu ni simulizi za wakufunzi wa hili kulunzi//
twende kazi kama unajua ku-kwea mnazi//
hili ni nyundo la kijambazi kaa wazi nikupe kazi//
husipende siasa wakati hauna darasa//
sawa kupenda anasa na kelele wakati huna kinasa//
huna thamani na karata yako garasa//
wee we wee weee kaa kimya tena fyata mkia//
tunapopita amkia huna sifa utakula vilivyo bakia//
unajaribu tunisha msuli kwa ugali kiporo na dagaa mbili//
unakuja umevaa msuli na kutunisha zako mbavu mbili//
kijana mdogo mvua mawingu yake dalili//
hapa tutakupembua tukubakizie punje mbili//
karibu dsm tufunze japo kiswahili//
utapate sema nasi tukusajili//
"Guys don pretend keep it real so dat kids can learn n grow from us"

Quertzal a.k.a lyrical blower





1 user(s) are reading this topic

0 members, 1 guests, 0 anonymous users